Arusha. Wanariadha wa Tanzania wametamba katika michuano ya John Stephen Akhwari international Marathon baada ya kuwashinda Wakenya.
Mashindano hayo yaliyofanyika leo Jumapili Juni 9, 2019, Mwanariadha Emmanuel Giriki alishinda kwa upande wa wanaume na Failuna Abdi kwa wasichana kushika nafasi za kwanza na kuwaacha mwanariadha kutoka nchi jirani ya Kenya katika mbio za umbali wa kilomita 21.
Giriki ambaye anatoka jeshi la wananchi ametumia muda wa saa 1:01:50 huku Failuna kutoka klabu ya winning spirit akitumia muda wa Saa 1:12:20.
Kwa upande wa wasichana mshindi wa pili Judith Cherolo kutoka Kenya na nafasi ya tatu Magdalena Chrispin wa Tanzania.
Wavulana mshindi wa pili mshindi wa pili Stivin Huche na wa tatu Michael Joseph wote watanzania.
Kwa upande wa kilomita tano, Watanzania wameongoza kwa upande wa wavulana na mshindi ni Marko Sylivesta, nafasi ya pili imechukuliwa na Mathayo Sombi na nafasi ya tatu ni Michael Kishindi.
Pia Soma
- Wachimbaji wa madini wafukiwa na kifusi Gairo
- Aliyewahi kuwa RPC Zanzibar akutwa amekufa nje ya nyumba yake
- Azaki 154 zapatiwa Sh11.7bilioni kutekeleza miradi ya maendeleo
Katika mashindano hayo ambayo yanashirikisha wanariadha zaidi ya 700 katika mbio za kilomita 21, kilomita 5 na kilomita Moja, Mgeni rasmi ni Waziri wa Habari, Utamaduni na Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe.