Wanachama wa klabu ya Yanga wameendelea kumimika katika ukumbi wa wa DYCC na mpaka saa 4:00 asubuhi robo tatu ya viti vya ukumbi vilikuwa vimejaa huku wanaoruhusiwa kuingia ndani ya ukumbi ni wale tu wanachama waliohakiki kadi zao mlangoni.
Kaimu katibu mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha na katibu mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wilfred Kidau ambao ni miongoni wa waalikwa kwenye mkutano huo amewasili na moja kwa moja wamekwenda kukaa meza kuu.
Ndani ya ukumbi wa DYCC, hawaruhusu mwananchama kuingia bila kuvaa barakoa ambazo zinagawiwa.
Wakati wanachama wakiendelea kumiminika katika ukumbi huo, hali imeendelea kuwa ya utulivu