SUPASTAA wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz @diamondplatnumz amekabidhiwa jezi na timu kubwa ya Duniani ya Washington Football Team @washingtonnfl ya Amerian Football
Diamond amekabidhiwa jezi hiyo iliyoandikwa "#PLATNUMZ" na namba 99 mgongoni ikiwa ni ishara ya kuthaminiwa na timu hiyo kubwa Duniani.
Kupitia ukurasa wao wa Instagram @washingtonnfl wamethibitisha hilo kwa kupost picha za Mondi akiwa na jezi yao ikiambatana na ujumbe ujumbe uliosomeka
"@diamondplatnumz repping the Burgundy & Gold." - Washington NFL
Timu ya #Washingtonnfl inashikilia nafasi ya pili (2) kwenye Ligi ya mpira wa Marekani
Diamond kwa sasa yupo nchini Marekani kwa ajili ya tour yake ya muziki (#diamondplatnumzusatour2021) ambapo anatarajia kwenda kupiga shoo Minnepolis kesho Ijumaa, October 15 na Denver, October 16, Jumamosi)