Baada ya kikosi cha Manchester City kutwaa taji lake la kwanza kikiwa chini ya kocha wake raia wa Hispania, Pep Guardiola kwakuifunga Arsenal kwa jumla ya mabao 3 – 0 makocha wa pande zote mbili wamezungumzia mchezo huo.
Kwa upande wa Arsene Wenger ameipongeza City kwa ubingwa huo huku akilaumu bao la pili kuwa lilikuwa ni la ‘offside’.
Pongezi kwa City kutwaa kombe, watarejea nyumbani wakiwa na furaha nasi tutarejea tukiwa tumepoteza.Kwa upande wa meneja wa Man City Pep Guardiola amesema kuwa
Najiskia vibaya lakini najua tuna stahili kuadhibiwa kwakuwa tumepoteza nafasi na tumewapatia ushindi, goli la kwanza lilikuwa sahihi lakini lapili lilikuwa ‘offside’ kwa vile nilivyoona mimi.
City waliweza kuutawala mchezo na kufanikiwa kuibuka na ushindi nawapongeza kwa hilo.Wakati unapopoteza mchezo kama huu kila mtu huoji kuhusu wachezaji, timu na mambo binafsi.
Lakini tumecheza na timu bora huwezi kusema walikuwa wakawaida.
Katika kipindi cha kwanza hatukuwa vizuri na tulifanya makosa mengi lakini kipindi cha pili tulirejea katika mchezo.Lilikuwa muhimu kutwaa taji hili baada ya kutolewa katika michuano ya FA Cup na sasa tunaangazia taji la ligi tunahitaji kulitwaa na tunataka kuingia robo faibnali ya Champions League.
Ushindi huu siyo wa kwangu bali ni kwa Manchester City wote