Washiriki wanawake wa mbio za baiskeli mkoa wa shinyanga wameiomba serikali na wadau wa michezo nchini kutoa kipaumbele na vifaa wezeshi kwa wanawake wanaoshiriki mbio baiskeli ili kuwawezesha kushiriki kwenye mashindano makubwa na kuitangaza nchi kupitia mchezo huo.
Washiriki wanawake wa mbio za baiskeli mkoa wa shinyanga wameiomba serikali na wadau wa michezo nchini kutoa kipaumbele na vifaa wezeshi kwa wanawake wanaoshiriki mbio baiskeli ili kuwawezesha kushiriki kwenye mashindano makubwa na kuitangaza nchi kupitia mchezo huo. Wakizungumza na Vyombo vya Habari wakati wa mashindano ya mbio za baiskeli yaliyofanyika katika uwanja wa CCM kambarage yaliyowakutanisha waendesha baiskeli kutoka sehemu mbalimbali mkoani humu wameeleza changamoto wanazokumbana nazo ikiwemo ukosefu wa baiskeli za kisasa na vifaa kwa ajili ya michezo hiyo.