Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya washinda medali 3 Paris 2024

Polish 20240806 092134075.png Wakenya washinda medali 3 Paris 2024

Tue, 6 Aug 2024 Chanzo: Bbc

Beatrice Chebet wa Kenya alishinda medali ya dhahabu katika mashindano ya Olimpiki mbio za mita 5,000.

Amekuwa miongoni mwa wanawake mjini Paris baada ya kushinda mbio hizo ambazo zilimfanya bingwa wa mita 1500 Faith Kipyegon kupokonywa medali ya fedha kabla ya kurejeshewa.

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 24 alivuka utepe katika dakika 14 na sekunde 28.56 mbele ya Kipyegon aliyechukua nafasi ya pili.

Kipyegon awali alinyang'anywa medali yake ya fedha baada ya kudaiwa kumzuia mwanariadha wa Ethiopia Gudaf Tsegay walipogongana katika kinyanganyiro hicho cha mita 5000.

Hata hivyo, Kipyegon hatimaye alirejeshewa medali hiyo baada ya kulalamika kwa mamlaka.

Wakati huohuo bingwa wa mbio za mita 800 Mkenya Mary Moraa alishinda medali ya shaba katika fainali ya mita 800 kwa wanawake, huku Tsige Duguma wa Ethiopia akishinda fedha nyuma ya Keely Hodgkinson wa Uingereza aliyenyakuwa dhahabu katika mbio hizo.

Chanzo: Bbc