Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vita ya fedha Manchester City dhidi ya Paris St-Germain kunasa saini ya Boateng

9847 5a05941b2ee40ff691000018 TZWeb

Sun, 24 Jun 2018 Chanzo: bongo5.com

Klabu ya Manchester City ya nchini Uingereza ipo kwenye vita kubwa dhidi ya matajiri wa Ufaransa timu ya Paris St-Germain kila moja ikijaribu kuwania saini ya beki wa Bayern Munich, Jerome Boateng.



Kwamujibu wa Sport Bild – Manchester Evening News,  Manchester City inavutiwa na Jerome Boateng na klabu ya Bayern Munich imejiandaa kusikiliza ofa itakayoletwa na mabingwa hao wa Uingereza kwaajili ya beki huyo ambaye kwa sasa yupo nchini Urusi kwenye michuano ya kombe la dunia.

Chanzo hicho kimeeleza kuwa Paris Saint-Germain nayo imeonyesha nia ya kumuhitaji mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 na hivyo City watalazimika kuchangamka ndani ya wiki hizi kama inamuhitaji kweli.

Mabingwa wa wa ligi ya Bundesliga wapo tayari kusikiliza ofa yoyote itakayo fika mezani kwao dau la kuanzia euro milioni 50 hadi 60.

Loading...
Chanzo: bongo5.com