WACHEZAJI Herieter Makambo na Meddie Kagere wamegeuka kuwa nyota wanaotajwa kabla ya mchezo wenyewe kuanza.
Mwanaspoti lilifika mapema uwanjani hapo na kuangalia namna ambavyo mashabiki wamejitokeza asubuhi hii katika Uwanja wa Taifa ndipo wachezaji hao wakawa wanatajwa mara kwa mara.
Kwa upande wa Mashabiki wa Yanga wao walikuwa wakimtaja Makambo kwamba atapeleka kilio kwa Simba kutokana na spidi yake aliyonayo katika Ligi.
Mashabiki wa Simba wao walikuwa wakimtaja mshambuliaji wao Meddie Kagere kwamba atamaliza shughuli yq kupeleka kilio kwa Yanga mapema.
Washambuliaji hawa wanakimbizana kwa magoli mpaka hivi sasa baada ya Kagere kufunga magoli 3 huku Makambo akifunga mawili.