Katika harakati za kunyanyua mpira wa miguu nchini Tanzania Kampuni ya kubashiri ya SportPesa imewatengeneza wataalamu ambao ni wazawa wakutengeneza (Pitch) nzuri za viwanja vya mpira wa miguu.
Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa, Abbas Tarimba
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa, Abbas Tarimba leo alhamisi jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Tarimba amesema ili mpira wetu ukue ni lazima tuwe na viwanja vizuri kwani uwanja ukiwa mbovu usitegemee kuwa na timu yenye uwezo mkubwa.
Kwa upande mwingine Tarimba ameiomba serikali na timu za soka kuchangamkia wataalamu hao kuwatumia katika kurekebisha viwanja vyao ili waweze kuwa na viwanja vya kisasa kama ulivyo uwanja wa Taifa. Tazama video yake hapa chini