Timu ya Taifa ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 ya Tanzania'Serengeti Boys' imechapwa mabao 5-0 na wenyeji Uturuki katika michuano ya UEFA Assist inayofanyika nchini humo.
Huo unakuwa mchezo wa pili Serengeti Boys kupoteza katika michuano hiyo baada ya ule wa kwanza kufungwa na Guinea bao 1-0 huku mchezo wa pili wakiibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Australia .
Serengeti Boys ilionekana kucheza kwa kiwango cha kawaida katika mchezo huo huku safu ya kiungo ikionekana kushindwa kuleta muunganiko mzuri na washambuliaji.
Washambuliaji wa Serengeti Boys wakiongozwa na Kelvin John walionekana kushindwa kufanya maamuzi pindi wanapolifikia lango la wapinzani wao na kujikuta wakipiga chenga zisizo na faida na mwisho kupokonywa mipira.
Serengeti Boys ilipangwa Kundi A katika michuano hiyo pamoja na wenyeji Uturuki,Guinea na Australia wakati kundi B lina timu za lCameroon, Uganda, Morocco na Belarus na Kundi C lina timu za Senegal, Nigeria, Angola na Montenegro.
Tanzania inatumia michuano hiyo kwa ajili ya kujiandaa na Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 ambayo yatafanyika hapa nchini kuanzia April 14 hadi 28 jijini Dar es Salaam.