Baada ya kuwepo kwa sintofahamu juu ya akaunti za Mtangazaji nguli wa habari za michezo nchini Tanzania ndugu Maulid Kitenge na kuwa hazipatikani kweye mtandao wa Instagram mapema asubuhi ya leo ameweka wazi kila kitu kuhusu akaunti hizo na kusema zimechukuliwa.
Akizungumza katika moja ya mahojiano yake aliyofanya asubuhi ya leo katika kituo cha habari ambacho anakifanyia kazi kwasasa Kitenge amesema baada ya kuanza mchakato wa kurudi kwenye kituo chake hicho cha awali akaunti zake mbili za instagram zilichukuliwa.
Aidha kitenge ameongeza kwa kusema kuwa hajatendewa haki kwani akaunti hizo ni sehemu nyingine anayotumia kupata riziki, ” mimi sijui ni nani amefanya kitendo hicho, nasikia watu wengi wakihusisha watu lakini mimi sijui ni nani amefanya hivyo ”
Hata hivyo kitenge amebainisha kuwa kwasasa hana akaunti Instagram na ahadi kuziridisha akaunti hizo.
Mtangazaji Maulid Kitenge amerudi EFM baada ya kuachana na kituo cha redio cha WasafiFm alichokuwa anafanyia kazi.