Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

"Unaikumbuka saa 7 mchana" - Simba SC

SIMBA "Unaikumbuka saa 7 mchana" - Simba SC

Wed, 20 May 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Klabu ya Simba SC, imetangaza kufanya jambo kubwa na la kihistoria siku ya Jumamosi Mei 23, 2020 ifikapo saa 7:00 mchana.

Simba SC imetangaza jambo hilo kupitia katika ukurasa wao wa mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo wameandika,

"Unaikumbuka saa 7 mchana, tukutane Jumamosi hii Mei 23, 2020. Historia mpya kwa klabu kaa tayari NguvuMoja"

Sasa kama unaikumbuka Saa 7 Mchana ilikuwa ni sera mpya ya Simba SC, ambapo walikuwa wanatumia wakati huo kutambulisha na kuwasaini wachezaji wao wapya, matukio makubwa au jambo lolote lililohusu klabu hiyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live