Wed, 20 May 2020
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Klabu ya Simba SC, imetangaza kufanya jambo kubwa na la kihistoria siku ya Jumamosi Mei 23, 2020 ifikapo saa 7:00 mchana.
Simba SC imetangaza jambo hilo kupitia katika ukurasa wao wa mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo wameandika,
"Unaikumbuka saa 7 mchana, tukutane Jumamosi hii Mei 23, 2020. Historia mpya kwa klabu kaa tayari NguvuMoja"
Sasa kama unaikumbuka Saa 7 Mchana ilikuwa ni sera mpya ya Simba SC, ambapo walikuwa wanatumia wakati huo kutambulisha na kuwasaini wachezaji wao wapya, matukio makubwa au jambo lolote lililohusu klabu hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live