Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ukata wamkimbiza kocha Arusha FC

26874 Pic+ukata TanzaniaWeb

Tue, 13 Nov 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha.  Athari ya Ligi Daraja la Kwanza kukosa mdhamini imeanza kuiathiri Arusha FC, baada ya Kocha Martin Mahimbo kuikacha timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza.

Akizungumza jana,  Mahimbo alisema ameacha kazi kwa kuwa klabu hiyo imeshindwa kumpa mkataba kutokana na ukata.

Alisema ameshindwa kuendelea na kazi kwa kuwa hajui hatima yake licha ya kuiongoza Arusha katika mechi mbili dhidi ya Geita Gold Mine na Ruvu Shooting ambapo alivuna pointi mbili.

“Nilifanya usajili kwa baadhi ya wachezaji kuwatoa Dar es Salaam na wengine Arusha na tulianza ligi vizuri ugenini, lakini baada ya kurejea hali ilikuwa ngumu na malalamiko ya wachezaji yalizidi nimeamua kuondoka,” alisema Mahimbo.

Katibu Mkuu wa Klabu hiyo, Frederick Lyimo alisema Mahimbo na wachezaji watatu wameondoka kutokana na kukosa fedha za uendeshaji.

Arusha FC ina pointi tatu baada ya kucheza mechi sita, imefungwa tatu na kutoka suluhu michezo mitatu, katika msimamo wa Ligi Daraja la Kwanza.



Chanzo: mwananchi.co.tz