Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ufunguo wa Oscar Piastri anao Fernando Alonso?

Image Oscar Piastri

Sun, 5 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kupata nafasi kwa Oscar Piastri kwenye Formula 1 kunamtegemea kwa kiasi fulani Fernando Alonso.

Hii ni kwa mujibu wa Marcin Budkowski, mkurugenzi mtendaji wa Alpine ambaye anakiri kwamba Piastri inayosimamiwa na Mark Webber inaungwa mkono kikamilifu na timu inayomilikiwa na Renault.

Piastri, raia wa wa Australia ambaye anaongoza msimamo wa Formula 2, tayari amesaini kama dereva wa akiba wa Alpine kwa mwaka 2022.

“Tutamfanyia mpango wa majaribio kwenye magari ya Formula 1, ili kuhakikisha kwamba kweli anapanda daraja. Tutamkuza Oscar sana, zaidi ya kumpeleka kwenye mbio kama dereva wetu wa tatu.”

Shida kwa Alpine ni kwamba, huku Esteban Ocon akiwa tayari amesainiwa na mkataba wake ukiwa unadumu hadi mwisho wa 2024, hatua ya Piastri kupanda daraja inaonekana kutegemea hatua inayofuata ya lejendari wa F1 Alonso, 40.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live