Thu, 26 Apr 2018
Chanzo: bongo5.com
Nusu fainali ya pili ya klabu bingwa barani Ulaya imeendelea tena usiku wa jana kwenye uwanja wa Allianz Arena.
Katika mchezo huo wenyeji Bayern Munich wamekubali kuendelea kupokea kichapo kutoka kwa Real Madrid baada ya kufungwa ka mabao 2-1.
Magoli ya Madrid yalifungwa na Marcelo dakika ya 44 na Marco Asensio (57), wakati bao la kufutia machozi la Bayern lilifungwa na Joshua Kimmich dakika ya 28.
Kwa sasa unasubiriwa mchezo mwingine wa nusu fainali ambao utawakutanisha miamba hiyo katika uwanja wa Santiago Bernabéu wiki ijayo.
Chanzo: bongo5.com