Tue, 13 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Shirikisho la soka nchini (TFF), limemtangaza kiungo wa klabu ya Yanga raia wa DR Congo, Papy Kabamba Tshitshimbi kuwa mchezaji bora wa mwezi Februari ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Tshitshimbi ametwaa tuzo hiyo baada ya kutupia mabao matatu na kukisaidia kikosi chake cha Yanga kuibuka na alama 12.
Katika kinyang’anyiro hicho Tshitshimbi ameshindana na Pius Buswita wa Yanga SC na Emmanuel Okwi wa Simba SC.
Kawaida mshindi wa tuzo hiyo huzawadiwa kitita cha milioni moja pamoja na king’amuzi cha Azam TV.
Chanzo: bongo5.com