Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tandahimba yamgeuzia kibao Bwire, yaipapasa Ruvu Shooting

12134 Ruvu+pic TanzaniaWeb

Thu, 16 Aug 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

 Mtwara. Ubovu wa uwanja wa Makonga, umetajwa kuwa  sababu iliyowafanya  Ruvu Shooting kufungwa  kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Tandahimba.

Ruvu Shooting wamepoteza mchezo huo wa kirafiki kwa mabao 2-1 mbele ya wanachama wao wapya 183.

Kocha wa maafande hao, Abdulmutik Haji. alisema vijana wake walishindwa kuendana na ubovu wa uwanja huo.

"Vijana walicheza vizuri lakini tatizo lililotufanya kutoonyesha ubora wetu kwa kiwango cha juu zaidi ni uwanja.

" Pasi zetu nyingi zilikuwa zikikwama njiani lakini tumepata  mazoezi ya kutosha kutoka kwao nadhani kwa maandalizi haya, tutakuwa na msimu mzuri," alisema Haji.

Bao la Ruvu Shooting kwenye mchezo huo wa kirafiki lilifungwa na Fully Zully Maganga huku yale ya Tandahimba City yakifungwa na Sadati Mpochi.

Ruvu Shooting itauanza msimu ujao wa Ligi Kuu Bara kwa kucheza dhidi ya Ndanda kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Mabatini, Agosti 22.

Chanzo: mwananchi.co.tz