Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TFF yakanusha kuyafungia mashindano yasiyo rasmi

717 Wallace Karia 600x362 TZW

Thu, 28 Dec 2017 Chanzo: bongo5.com

Rais wa Shirikisho la Soka nchini TFF, Wallace Karia amesadikika kuwa ametoa kauli iliyoleta utata kuhusiana na zuio la mashindano ya soka yasiyo rasmi, ambapo TFF limetoa ukanusho wa taarifa hiyo na kufanya ufafanuzi wa ziada.

Shirikisho hilo la Soka nchini limeeleza kuwa alichosema Rais uyo ni kuhusiana na maandalizi ya kanuni ambazo zitatakiwa kufuatwa na waandaji wa mashindano madogo ya soka nchini na si zuio la mashindano kama ambavyo ilitafsiriwa na jopo la watu.

“TFF inaandaa kanuni ili mashindano yote ya aina hiyo yakidhi vigezo katika utaratibu mzuri na watapata vibali kupitia FA Wilaya na Mikoa baada ya kutimiza vigezo vitakavyowekwa”, imeeleza sehemu ya taarifa ya TFF.

Chanzo: bongo5.com