Sat, 15 Jun 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
SHIRIKISHO la Soka nchini (TFF) nao wametia timu katika hafla ya Kubwa Kuliko iliyoandaliwa na Klabu ya Yanga ambayo ina lengo la kuchangisha pesa zitakazotumika kwenye usajili wa msimu ujao.
TFFÂ imewakilishwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Ally Mchungahela ambaye ndiye aliyetambulishwa na Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Fredrick Mwakalebela.
Inadaiwa wageni waalikwa ambao walialikwa kutoka TFF wamepata udhuru baada ya kuumwa na wengine kuuguliwa.
Katika hafla hiyo mgeni rasmi ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye ameambatana na Mkuu wa Mkoa Paul Makonda.
Chanzo: mwananchi.co.tz