Thu, 4 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Kiungo wa Azam FC Salum Abubakar maarufu kama Sure Boy amepatwa na msiba mzito wa kufiwa na Mama yake mzazi.
Taarifa hizo zimetolewa na uongozi wa klabu hiyo ambapo wamesema msiba huo upo Magomeni jijini Dar es Salaam katika mtaa wa Lubusha na mazishi yatafanyika Alhamisi hii majira ya saa 10.
Hata hivyo bado haijhafahamika chanzo cha msiba huo.
Bongo5 tunatoa pole kwa msiba huo na pia tunamuombea roho ya marehemu ilazwe mahali pema peponi, Amiina.
Chanzo: bongo5.com