Thu, 25 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Klabu ya Mwadui FC imepoteza kocha wake msaidizi, Jumanne Ntambi ambaye amefariki dunia hapo jana siku ya Jumanne mjini Shinyanga.
Ntambi amefariki dunia katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga kufuatia kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo.
Enzi za uhai wake Ntambi amepata kuichezea timu ya Biashara Shinyanga na mpaka umauti unafika alikuwa akiitumikia klabu ya Mwadui FC.
Chanzo: bongo5.com