Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Swansea City yapata kocha mpya

734 DSIXkfCW4AE9QRv

Thu, 28 Dec 2017 Chanzo: bongo5.com

Klabu ya soka ya Swansea City ya nchini Uingereza imemtangaza rasmi Carlos Carvalhal kuwa ndio kocha wao mpya atakayekinoa kikosi hicho hadi mwishoni mwa msimu wa 2017/18.

Carlos Carvalhal ambaye alishawahi kuzinoa klabu za Besiktas, Sheffield Wednesday na Sporting Lisbon ataiongoza kwa mara ya kwanza Swansea dhidi ya Watford.

Taarifa rasmi kutoka kwenye mtandao wa klabu hiyo wa (www.swanseacity.com) umeeleza kuwa Kocha huyo alijiunga na Swansea jana usiku na akitokea likizoni nchini Ureno huku ikishindwa kueleza dau la usajili.

Maamuzi hayo yanakuja baada ya Desemba 21, 2017, klabu hiyo kumtimua kocha wake Paul Clement kwa kupoteza mechi 9 kwenye msimu huu katika michuano mbalimbali.

Chanzo: bongo5.com