Kartepe. Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Ausamms hataki utani unaambiwa.
Katika kuwaweka 'fiti' wachezaji ameamua kuwapigisha mazoezi kutwa mara mbili na baada ya hapo ni mapumziko.
Ambapo asubuhi wanafanya masaa mawili na nusu na jioni hivyo.
Ausamms anaamini programu hiyo itamsaidia na hataki mchezaji kujianzishia program yake tofauti na hiyo na baada ya hapo ni mapumziko kwa sababu mazoezi ni makali.
Kutokana na hilo, licha ya viwanja wanavgotumia kiwa karibu na hoteli amehakiki wanakwenda kwa gari na kurudi.
Simba inaendelea na maandalizi yao nchini uturuki mpaka Agosti 5 watakapoanza safari ya kirudi Tanzania.