Thu, 23 Aug 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Admini msaidizi wa Simba Sport folever, aliyetambulika kwa jina moja la Kilambakime akimkabidhi kiasi cha shilingi laki moja kiungo wa Simba, Hassan Dilunga kutokana na kuisaidia timu yake kutwaa ubingwa wa Ngao ya Jamii dhidi ya Mtibwa Sugar.
Mchezo huo ulichezwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na Simba waliibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Simba Ilicheza mechi hiyo ya Ngao ya Jamii kwa sababu ni bingwa wa Ligi Kuu Bara na Mtibwa ni mabingwa Kombe la Shirikisho.
Chanzo: mwananchi.co.tz