Sun, 19 Sep 2021
Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz
Kikosi cha timu ya vijana ya Simba U 20, imepata ushindi wa bao 1-0, dhidi ya JKU U 20, katika mechi ya kirafiki.
Bao la Simba lilifungwa na Andrew Michael kwa mkwaju wa penalti baada ya beki wa JKU kucheza rafu ndani ya boksi.
Simba wakipata bao hilo kipindi cha pili baada ya dakika 30, za kipindi cha kwanza kuisha kwa suluhu .
Mechi hiyo ilikuwa ya aina yake kwa Simba ambao walishambuliazaidi kuliko wapinzani wao JKU.
JKU wao walicheza kwa nidhamu na kupasiana pasi fupi fupi haswa eneo la katikati mwa Uwanja na kufanya mashambulizi machache.
Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz