Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba: Uchangiaji wa Uwanja Umetushangaza Sana

Try Again 01 Simba: Uchangiaji wa Uwanja Umetushangaza Sana

Tue, 21 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

KLABU ys Simba imefunguka kuhusu mwitikio mkubwa wa watu kuchangia ujenzi wa uwanja wao mpya wa mashindano ambao utajengwa huko Bunju.

"Tangu tumetangaza kuhusu kuchangia ujenzi wa uwanja wetu mwitikio siyo mbaya, imetushangaza sana, mwitikio ni mzuri, inaonyesha kuna morari kubwa kwa mashabiki, wanachama na wadau wetu, hivi karibuni tutakuja na utaratibu mpya ili wale watu wetu wa nje nao waweze kuchangia.

“Pia wale watakaochangia zaidi tutaweka utaratibu wa kuwatambua, tuendelee kusapoti, hivi karibini Bodi itatangaza kamati maalum kwa ajili ya mchakato huo wa michango.

“Kamati itakuja na mpango mkakati wote, ikiwemo bajeti, mchoro wa uwanja na kila kitu kinachohusiana na uwanja, vinginevyo watu waendelee kutuchangia kama tulivyotoa maelekezo ya awali.”

Kauli ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu ya Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ kuhusu mchakato wa kuchangia ujenzi wa uwanja wao mpya mali ya klabu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live