Mon, 12 Feb 2018
Chanzo: bongo5.com
Kocha Mkuu wa klabu ya Simba SC, Pierre Lechantre tayari ameshatangaza kikosi cha maangamizi ambacho kinaivaa klabu ya Gendamarie Tnale kutoka Djibouti kwenye mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho barani Afrika.
Simba SC ambao hao ndio watakuwa nyumbani kunako dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam wataanza na wachezaji wao muhimu kwa kutumia mfumo wao wa 3-5-2 ambapo John Bocco na Emmanuel Okwi wataongoza mashambulizi.
Chanzo: bongo5.com