Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba SC yarejea Dar na dawa ya Singida United

1452 Simba SC.png TZW

Thu, 18 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Kikosi cha Simba leo asubuhi kimeanza safari ya kurejea jijini Dar es Salaam tayari kwa mchezo wake dhidi Singida United kikitokea Mkoani Morogoro ambako kiliweka kambi yake kwaajili ya maandalizi ya Vpl.



Kikosi cha Simba kikiwa chini ya kocha wake, Masoud Djuma kitashuka katika Uwanja wa Taifa huku kikiwa na nyotawake mshambuliajia raia wa Uganda, Emmanuel Okwi ambaye alikuwa akisumbuliwa na majeraha.

Simba SC inaongoza katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania Bara kwa kuwa na alama 26 sawa na wanalambalamba klabu ya Azam FC wakiwa na tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.

Nafasi yatatu ikishikiliwa na Mtibwa Sugar wenye pointi 24 ya nne ikiwa chini ya Singida United na yatano wakishikilia mabingwa watetezi Young Africans wenye alama 21.

Chanzo: bongo5.com