KIPA wa Bandari anayetakiwa na Yanga, Farouk Shikalo amemuangalia beki Kelvin Yondani kisha akasema jamaa kazi anaijua.
Akizungumza na gazeti hili, Shikalo alisema Yondani ni beki hasa kutokana na akili yake ya kukabiliana na washambuliaji.
Shikalo alisema kama atajiunga na Yanga kisha kucheza pamoja na beki huyo kazi itakuwa nzuri kutokana na uimara wa mkongwe huyo.
Alisema kama isingekuwa uimara wa Yondani, David Mwantika na kipa Aishi Manula, Stars ingepigwa mabao mengi.
Alisema anachopenda kwa Yondani ni utulivu wake na kucheza kwa hesabu kali, mambo yaliyompa ubora katika mchezo huo wa juzi licha ya kupoteza.
“Leo (juzi) ndiyo mara ya kwanza kumuona kwa macho anacheza huyu Yondani (Kelvin) ni beki hodari sana anajua sana nimempenda,” alisema Shikalo.
Pia Soma
- Kamusoko awashangaa Stars
- Umakini, pumzi vimeigharimu Taifa Stars Misri
- Ajibu aikamua Simba Milioni 100/-