Mon, 26 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Beki kisiki wa klabu ya ska ya Real Madrid, Sergio Ramos na mpenzi wake Pilar Rubio wamefanikiwa kupata mtoto wao wa tatu.
Ramos amethibitisha hilo kupitia mtandao wa Instagram ambapo ameweka picha akiwa na Pilar na mtoto wao huyo na kuandika, “We are very happy to introduce you to Alejandro, born today at 6:24PM, 3.1kg. Thank you for sharing our joy. I love you Pilar Rubio.”
Mtoto huyo alizaliwa jana (Jumapili) akiwa na uzito wa 3.1kg na tayari amepewa jina la Alejandro.
Mtoto huyo anaungana na kaka zake wengine wawili akiwemo Sergio Jr (3) na Marco (2).
Chanzo: bongo5.com