UONGOZI wa klabu ya Simba umemteua Rispa Hatibu kuwa msaidizi wa Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo, Senzo Mazingisa. Uteuzi huo unakuja baada ya Mazingisa kutokuwa na msaidizi tangu alipotambulishwa kuwa Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo Septemba mwaka huu. Wakati huo huo, taarifa iliyotolewa na kurugenzi huyo ilieleza kumteua Hashim Mbaga kuwa Mkuregenzi wa Wanachama na Mashabiki. "Tunawakaribisha klabuni tukiwa na matarajio ya kuiwezesha klabu kupiga hatua na kuhakikisha kuwa jukumu la mabadiliko linafanikiwa," ilieleza taarifa hiyo. Taarifa hiyo ilieleza zaidi kwamba uteuzi huo ulianza kazi mapema tangu Oktoba Mosi mwaka huu.
UONGOZI wa klabu ya Simba umemteua Rispa Hatibu kuwa msaidizi wa Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo, Senzo Mazingisa. Uteuzi huo unakuja baada ya Mazingisa kutokuwa na msaidizi tangu alipotambulishwa kuwa Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo Septemba mwaka huu. Wakati huo huo, taarifa iliyotolewa na kurugenzi huyo ilieleza kumteua Hashim Mbaga kuwa Mkuregenzi wa Wanachama na Mashabiki. "Tunawakaribisha klabuni tukiwa na matarajio ya kuiwezesha klabu kupiga hatua na kuhakikisha kuwa jukumu la mabadiliko linafanikiwa," ilieleza taarifa hiyo. Taarifa hiyo ilieleza zaidi kwamba uteuzi huo ulianza kazi mapema tangu Oktoba Mosi mwaka huu.