Timu ya taifa ya Senegal leo imerudisha matumaini ya Waafrika kunako michuano ya kombe la Dunia kwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Poland .
Goli la kwanza la Senegal limepatikana kwa beki wa Poland, Thiago Cionek kujifunga kunako dakika ya 37 huku goli la pili la likitupiwa na Mbaye Niang.
Goli pekee la kufutia machozi la Poland inayoongozwa na Lewandowski likifungwa na Grzegorz Krychowiak kunako dakika ya 86 ya mchezo.
Senegal inakuwa timu ya kwanza kutoka bara la Afrika kupata ushindi kwenye michuano ya kombe la dunia ya mwaka huu nchini Urusi.
Je, Senegal ya mwaka huu inaweza kuvunja rekodi yao ya mwaka 2002 ya kufika robo fainali ya michuano hiyo ya Kombe la dunia? toa maoni yako