Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Samatta aisaidia KRC Genk kufika Fainali

2765 Krch 658x400

Wed, 7 Feb 2018 Chanzo: millardayo.com

Usiku wa February 7, 2018 mshambuliaji wa kimataifa kutoka Tanzania anayecheza Soka nchini Ubelgiji katika Klabu ya KRC Genk Mbwana Samatta akiwa na klabu hiyo usiku wa leo wamefanikiwa kutinga fainali ya Kombe la Ubelgiji baada ya kushinda mchezo wa nusu fainali dhidi ya Kortrijk.

Katika mchezo huo Samatta amecheza dakika zote 90 na kuisaidia timu yake kushinda goal 1-0 katika nusu fainali ya pili hivyo kufanya matokeo ya jumla kuwa 3-3 na Genk kufuzu kwa faida ya goli la ugenini baada ya Genk kupoteza 3-2 kwenye nusu fainali ya kwanza.

Bao la Genk limefungwa na kiungo Ibrahima Seck ambaye ni Msenegali katika dakika ya 15 akimalizia pasi ya Mhispania Alejandro Melero.

MAKOCHA WA YANGA NA NJOMBE MJII BAADA YA GAME KUMALIZIKA, BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUTAZAMA

Chanzo: millardayo.com