Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Samatta afananishwa na Drogba Genk

58782 Pic+samatta

Tue, 21 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Kiungo wa Ghana, Joseph Paintsil amesema Mbwana Samatta ni mshambuliaji wa aina yake na mabao aliyofunga yamechangia kwa kiasi kikubwa kuipa ubingwa wa Ligi Kuu Ubelgiji KRC Genk.

KRC Genk juzi usiku ilikabidhiwa ubingwa wa Ligi Kuu ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa Luminus, baada ya kucheza na Standard Liege katika mchezo wa kukamilisha ratiba waliotoka suluhu.

Akizungumza kwa simu jana, Paintsil alisema amejifunza mengi kutoka kwa Samatta na kila mmoja ana furaha naye kwa kuwa amefanya kazi kubwa msimu huu 2018/2019.

Paintsil alisema ana kipaji cha kufunga mabao kwa mpira wa kichwa kama aliyekuwa mshambuliaji wa Chelsea na Ivory Coas, Didier Drogba.

Samatta amekuwa akifunga mabao ya kichwa kutokana na mipira krosi inayopigwa na kiungo wa pembeni, Leandro Trossard, ambaye amekuwa akimtengenezea nafasi za kufunga.

“Ninachoweza kumtofautisha Samatta na washambuliaji wengine ni namna ya uchezaji wake, ana staili tofauti, anaweza kusimama mbele, anaweza kuwa mshambuliaji lakini pia akatokea pembeni,” alisema.

Pia Soma

Samatta amemaliza msimu wa Ligi Kuu Ubelgiji akiwa ndiye mfungaji bora wa KRC Genk na alishika nafasi ya pili katika orodha ya wachezaji waliokuwa wakiwania tuzo ya mfungaji bora. Hamdi Harbaoui wa timu ya Zulte Waregem aliyempiku Samatta kwa mabao mawili akifunga 25.

Samatta aliwahi kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka mwenye asili ya Afrika anayecheza soka la kulipwa Ubelgiji.

Tuzo hiyo ya pili kwa Samatta, mara ya kwanza alitwaa Januari 2016, Abuja, Nigeria alikotangazwa mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani wakati akijiandaa kuondoka TP Mazembe ya DR Congo kwenda KRC Genk. Genk imepata tiketi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Chanzo: mwananchi.co.tz