Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sababu za Neymar kushindwa kufika uwanjani hizi hapa

143 Skysports Neymar Psg Neymar Paris 4079160 660x400 TZW

Thu, 14 Dec 2017 Chanzo: millardayo.com

Club ya Paris Saint Germain ya Ufaransa imeweka wazi sababu za kutokuwa na mpango wa kumtumia mchezaji wao wa kimataifa wa Brazil Neymar wakati wa mchezo wa leo wa Ligi Kuu Ufaransa dhidi ya Strasbourg.

Kocha wa PSG Unai Emery amethibitisha kuwa hawatokuwa na Neymar wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Ufaransa wakiwa ugenini dhidi ya Strasbourg kutokana na staa huyo kupewa ruhusa maalum ya kwenda kwao Brazil kushughukia matatizo yake ya kifamilia na atarudi baada ya siku tatu hadi nne.

Hata hivyo Neymar ambaye ni mchezaji ghali zaidi duniani kwa sasa kutokana na kusajiliwa na PSG kwa dau la pound milioni 199 akitokea FC Barcelona, aliukosa mchezo wa weekend iliyomalizika wa PSG dhidi ya Lille uliyomalizika kwa PSG kupata ushindi wa magoli 3-1 kutokana na kutumikia adhabu.

VIDEO: Atayofanya Mo Dewji kwa Simba ndani ya mwaka mmoja

Chanzo: millardayo.com