Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ronaldo hazuiliki, ajitengenezea rekodi mpya kwenye soka

5003 4A53A3BE00000578 5515937 Image A 65 1521404593628 TZW

Mon, 19 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Mshambuliaji hatari wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amezidi kujitengenezea rekodi katika timu hiyo.



Usiku wa jana mchezaji huyo amefanikiwa kufunga hat-trick yake ya 50. Katika mchezo huo ambao Madrid walicheza na Girona, Ronaldo alifanikia kufunga magoli manne katika ushindi wa mabao 6-3 ambao Madrid wameupata.

Ronaldo alifunga magoli hayo dakika ya 11, 47, 64 na 90 wakati magoli mengine yalifungwa na Lucas Vazquez dakika ya 59 na Bale kwenye dakika ya 86.

Wakati huo hu magoli ya Girona yalifungwa na Cristian Stuani, aliyefunga mabao mawili (29 na 67) na Juanpe (88).

Kwa sasa Ronaldo anashika nafasi ya pili kwa kufunga mabao kwenye La Liga msimu huu akiwa na mabao 22, wakati Lionel Messi akiongoza akiwa tayari ameshafunga mabao 25.

Chanzo: bongo5.com