Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Real Madrid wayaaga mashindano ya Copa del Rey kwa fedheha

1912 DUWwDlxU0AAxi8w TZW

Thu, 25 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Klabu ya Real Madrid imeyaaga mashindano ya kombe la mfalme nchini Hispania baada ya kukubali kichapo cha goli 2-1 dhidi ya vibonde Leganes.



Real Madrid wametolewa kwa faida ya magoli ya ugenini ambapo kwenye mchezo wa kwanza Madrid walishinda goli 1-0 ugenini kwahiyo jana wametolewa kwa kuruhusu goli 2-1  Santiago Bernabeu .

Matokeo mengine ya kombe hilo ni klabu ya Valencia dhidi ya Alaves ambapo Valencia walifungwa goli 2-1 Agregates (3-3) hata hivyo wamefuzu kwa changamoto ya penati 3-2 .

Hiki kinakuwa kipigo kingine cha fedheha kwa klabu hiyo ambapo kwa msimu huu Madrid wamepoteza mechi mbili uwanjani kwao Santiago Bernabeu.

Chanzo: bongo5.com