Klabu ya Real Madrid imeyaaga mashindano ya kombe la mfalme nchini Hispania baada ya kukubali kichapo cha goli 2-1 dhidi ya vibonde Leganes.
Real Madrid wametolewa kwa faida ya magoli ya ugenini ambapo kwenye mchezo wa kwanza Madrid walishinda goli 1-0 ugenini kwahiyo jana wametolewa kwa kuruhusu goli 2-1 Santiago Bernabeu .
Matokeo mengine ya kombe hilo ni klabu ya Valencia dhidi ya Alaves ambapo Valencia walifungwa goli 2-1 Agregates (3-3) hata hivyo wamefuzu kwa changamoto ya penati 3-2 .
Hiki kinakuwa kipigo kingine cha fedheha kwa klabu hiyo ambapo kwa msimu huu Madrid wamepoteza mechi mbili uwanjani kwao Santiago Bernabeu.