Wed, 1 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji wa zamani wa Arsenal na Liverpool, Ray Kennedy amefariki dunia Gwiji huyo amefariki jana Novemba 30 akiwa na umri miaka 71 baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Kennedy aling'ara akiwa na Arsenal kabla ya kuuzwa Liverpool kwa bei iliyovunja rekodi ya uhamisho.
Akafanya makubwa Liverpool ila akapata ugonjwa wa parkinson na kulazimika kustaafu. Ndoa yake ikavunjika na akauza medali zake ili ajitibu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live