Shirikisho la soka nchini TFF limethibitisha kuwa Tanzania itawakilishwa na timu nne kwenye michuano ya vilabu barani Afrika smimu ujao wa 2021-22 kwenye michuano ya klabu bingwa na kombe la shirikisho.
Submitted by Ibra Kasuga on Jumatatu , 21st Jun , 2021 Wachezaji wa Simba na Yanga wakiwania mpira kwenye moja ya michezo ya Ligi Kuu
Hii ni kufuatia Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi 12 za juu kisoka kwenye viwango vya ubora wa Ligi barani Afrika ambapo kikanunu mataifa 12 ya juu upeleka timu nne kwenye michuano ya CAF, mbili zitacheza klabu bingwa na mbili zitawakilisha kwa upande wa kombe la shirikisho.
Taarifa rasmi iliyotolewa na TFF ikithibitisha Tanzania kupeleka timu nne kwenye michuano ya vilabu barani Afrika msimu huu