Thu, 28 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kundi la Wanasarakasi la Ramadhani Brothers kutoka Tanzania wamemaliza katika nafasi ya tano kwenye shindano maarufu la Kusaka Vipaji la 'America's Got Talent' lililofanyika nchini Marekani.
Ramadhani walionesha Sanaa yao ya kushangaza mbele ya majaji wanne akiwemo Simon Cowell, Sofia Vergara, Heidi Klum na Howie Mandel ambapo Adrian Stoica ndiye aliyeibuka mshindi.
Kupitia ukurasa wao wa mitandao ya kijamii Ramadhani Brothers wameandika "Hatujapata kura za kutosha, tumekuwa watano katika shindano, na tunashukuru AGT kwa nafasi hii na watu wote waliotupigia kura, mapambano yanaendelea"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live