Mchezaji tennis raia wa Hispania, Rafael Nadal amerudi kwa kishindo kwenye mchezo huo baada ya kumshinda Muingereza, Philipp Kohlschreiber hapo jana kwenye michuano ya Davis Cup.
Nadal ambaye ni mchezaji namba moja kwenye viwango vya tennis duniani amemshinda Philipp Kohlschreiber kwa jumla ya seti 6-2 6-2 6-3 huu ukiwa ni mchezo wake wa kwanza akitoka kuuguza majeraha yaliyokuwa yakimsumbua tangu mwezi Januari wakati wa michuano ya Australian Open.
Ushindi huo unamfanya kushinda mara 23 mfululizo kwenye michuano hiyo ya Devis Cup hii ikiwa ni kwa mchezaji mmoja na zaidi ya mmoja.
Kwa ushindi huo aiwezesha timu yake ya Hispania ambao ndiyo wenyeji wa michuano hiyo ya Devis Cup kukutana na Ufaransa ama Italia.