Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Polisi yatumia mabomu kutawanya mashabiki Uwanja Taifa

48423 Pic+mashabiki

Mon, 25 Mar 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Polisi imetumia mabomu ya machozi kutawanya mashabiki waliokuwa wamepitia uwanja wa Uhuru baada ya mageti makubwa kujaa.

Mashabiki hao walielekezwa na watu wa Selcom kutokana na mageti kujaa, lakini baada ya msongamano kuwa mkubwa iliwalazimu polisi kutumia mabomu ya machozi.

Mabomu hayo yalisaidia kutawanya mashabiki waliokuwa wamekaa uwanja uhuru kiasi cha kukimbizana na kukanyagana.

Wingi wa mashabiki ulionekana mkubwa kuliko idadi ya mapolisi ambao wamejitokeza uwanjani hapa kiasi cha kutumia mabomu ya machozi kuwatanya.

TIKETI MTIHANI

Katika upande wa tiketi kulikuwa na changamoto baada ya kujitokeza idadi kubwa ya watu huku tiketi zikiwa chache.

Mashabiki wengi waliokuwa nje ya uwanja walisikika wakilalama juu ya ufinyu wa tiketi kiasi cha kujikuta wakizurura bila kuwa na msaada wowote.

 



Chanzo: mwananchi.co.tz