Klabu ya Manchester United imeongoza maelfu ya mashabiki kutoa heshima zao katika kumbukumbu ya watu 23 waliyofariki dunia kufuatia ajali ya ndege iliyotokea huko Munich miaka 60 iliyopita.
Meneja wa timu hiyo, Jose Mourinho pamoja na wachezaji wake walikuwepo katika viunga hivyo huku legendari wa Old Trafford, Sir Bobby Charlton ambaye alinusurika katika ajali hiyo ya Februari 6 mwaka 1958 akiwa ni miongoni mwa waliyohudhuria kwenye kumbu kumbu hiyo akiwa sambamba na Sir Alex Ferguson.
Katika kumbu kumbu hiyo iliongozwa na kukaa kimya kwa muda na kuimba mashahiri mbalimbali.
Picha zikiwaonyesha wachezaji wa Man United, mashabiki na baadhi ya waliyo wahikuihudumia timu hiyo
Wachezaji wa kikosi kilichopata ajali picha hii ikiwa ni kabla ya tukio hilo