Thu, 18 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Msanii wa P-Square Paul Okoye maarufu kama Rude Boy leo amepokea ugeni mkubwa nyumbani kwake mjini Lagos akiwemo mchezaji bora wa Afrika kwa upande wa wanawake, Asisat Lamina Oshoala ambaye anacheza timu ya taifa ya wanawake ya Nigeria na klabu ya Dalian Quanjian F.C ya Chini.
Paul Okoye akiwa na Asisat Oshoala (Kushoto) na Onome Ebi (kulia)
Katika ugeni huo Oshoala aliongozana na mchezaji mwenzake wa Nigeria, Onome Ebi ambaye anacheza ligi kuu ya Belarus.
Oshoala amewahi kuchezea timu kadhaa za wanawake za Uingereza ikiwemo Liverpool mwaka 2015 na Arsenal mwaka 2016.
Chanzo: bongo5.com