Mchezaji mpya wa Manchester United, Alexis Sanchez ameonekana kukagua jumba la kifahari katika jiji la Manchester ambalo atakuwa anaishi.
Inadaiwa kuwa mjengo huo una gharimu kiasi cha paund milioni mbili ambapo ni zaidi ya shilingi bilioni sita kwa fedha za kitanzania. Nyumba hiyo ina vyumba vitano ikiwemo chumba kimoja kikiwa ni chumba cha piano, uwanja wa mazoezi ya mpira wa miguu ambapo pia nyumba hiyo ipo karibu na nyumba ya golikipa wa Manchester City, Claudio Bravo.
Tangu mapema wiki hii mchezaji huyo alifikia katika hoteli ya Lowry iliyopo mjini Manchester akiwa pamoja na familia wakitokea London ambapo walikuwa wanaishi mwanzoni wakati Sanchez akicheza katika klabu ya Arsenal.