Wed, 14 Feb 2018
Chanzo: bongo5.com
Klabu ya soka ya Everton ni moja kati ya timu za soka duniani ambayo imekuwa zikisaidia kwa ukaribu jamii. Usiku wa jana timu hiyo ilisherehekea miaka 30 ya kufanya kazi katika jamii katika chakula cha jioni.
Sherehe hiyo ambayo imepewa jina la Gala Dinner, ilifanyika katika ukumbi wa St George’s Hall uliopo katika mji wa Liverpool, ilihudhuriwa na kocha wao Sam Allardyce pamoja na mastaa mbalimbali wa klabu hiyo akiwemo, Wayne Rooney, Theo Walcott, Cenk Tosun.
Chanzo: bongo5.com