Thu, 26 Apr 2018
Chanzo: bongo5.com
Kikosi cha klabu ya Atletico Madrid tayari kimetua mjini London jioni hii kwa ajili ya kucheza mchezo wao wa nusu fainali wa kombe la Europa League dhidi ya Arsenal.
Atletico wametua mjini hapo wakiwa na washambuliaji wao hatari Diego Costa na Fernando Torres ambao wote wanatarajiwa kucheza kwenye mchezo huo ikiwa ni mara yao ya kurudi tena Uingereza tangu walipoondoka.
Naye Antoine Griezmann ni miongoni mwa wachzaji ambao wamesafiri na timu hiyo. Tazama picha zaidi hapa chini.
Chanzo: bongo5.com