Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Operesheni Sanchez, Mourinho asisitiza kufunga mjadala na Arsenal baada ya kutua Old Trafford (+Picha)

1475 MOURN.png TZW

Thu, 18 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Meneja wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho amewasili katika uwanja wa Old Trafford siku ya Jumatano asubuhi huku ikiwa timu hiyo inakaribia kumsajili Alexis Sanchez.



Mourinho amewasili katika maeneo ya mazoezi ya Aon Training Complex wakati mazungumzo na Arsenal yakiendelea ya dau la paundi milioni 35 kunasa saini ya mchezaji wa kimataifa wa Chile, Sanchez.



 

Baadhi ya wacheza wa klabu hiyo wameonekana kuwasili makao makuu ya timu hiyo akiwemo Martial,ambaye alikuwa wakwanza kufunga bao siku ya Jumatatu usiku dhidi ya Stoke na kuchomoza na ushindi wa mabao 3-0.

Marcus Rashford, Juan Mata, Scott McTominay, Daley Blind na Sergio Romero piia wameonekana kuwasili akiwemo na Mcameron, Borthwick-Jackson ambaye amerejea kutoka kwa mkopo Leeds United.



Marcus Rashford akiwasili Aon Training Complex



Anthony Martial akiendesha gari akiwasili Old Trafford baada ya kuisaidia timu yake mbele ya Stoke

Sergio Romero akiwasili makao makuu CarringtonĀ 







Mcameron, Borthwick-JacksonĀ  akiwasili baada ya kurejea kwa mkopo Leeds

Chanzo: bongo5.com