Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Okagbare Afungiwa Miaka 10 Kushiriki Riadha

Okagbare Mwanariadha wa Nigeria Blessing Okagbare

Sun, 20 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwanariadha wa Nigeria Blessing Okagbare amesimamishwa kwa muda wa miaka kumi kwa ukiukaji wa sheria nyingi za kupinga matumizi ya dawa za kuongeza nguvu mwilini.

Kitengo cha Uadilifu cha Riadha (AIU) kimetangaza: “Miaka mitano kwa uwepo na matumizi ya dawa nyingi zilizopigwa marufuku na miaka mitano kwa kukataa kushirikiana na uchunguzi wa AIU. ”

Blessing Okagbare alikuwa mshindi wa medali ya fedha katika Michezo ya Olimpiki ya mwaka 2008, katika mashindano ya dunia ya mwaka 2013, na kututunukiwa katika mashindano mengi ya Afrika.

Okagbare alisimamishwa kwa muda katikati ya Michezo ya Olimpiki ya Tokyo 2021, siku chache baada ya kuthibitishwa kuwa na chembe chembe za madawa ya kusisimua mwili.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live