Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

O.J. Simpson afariki Dunia

O.J. Simpson O.J. Simpson.

Fri, 12 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mchezaji wa zamani wa NFL na mtangazaji, Orenthal James Simpson amefariki Dunia kwa saratani akiwa na umri wa miaka 76.

Umaarufu na mafanikio ya O.J. Simpson yalifunikwa na kuachiliwa kwake katika mauaji ya kikatili ya mke wake wa zamani, Nicole Brown Simpson na rafiki yake Ron Goldman.

Orenthal James Simpson mzaliwa wa San Francisco alijipatia umaarufu kama Mchezaji wa Chuo Kikuu kabla ya kucheza katika NFL.

Mnamo 1995 aliachiliwa huru baada ya kukutwa hana hatia kwa mauaji ya mke wake wa zamani Nicole Brown na rafiki yake katika kesi ambayo ilitikisa Marekani.

Mnamo 2008, O.J. Simpson alihukumiwa kifungo cha miaka 33 kwa makosa ya wizi wa kutumia silaha kabla ya kuachiliwa mnamo 2017.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live